Saturday, November 14, 2009

TARIFA ILIYOTUFIA KATIKA BLOG YETU YA MICHEZO MCHAKAMCHAKA WA KUTINGA FAINALI KOMBE LA DUNIA 2010 IYOOO!!! Afrika kujua leo Nchi 3 zitakazoungana na Wenyeji Afrika Kusini, Ghana na Ivory Coast Fainali!!!
Wakati Bara la Afrika leo linategemewa kuzipata Nchi 3 zitazojumuika na Afrika Kusini, Ghana na Ivory Coast Fainali Kombe la Dunia huko Afrika Kusini kuanzia Juni 11 mwakani, Mabara ya Ulaya na Marekani leo wanacheza mechi zao za kwanza na kurudiana Jumatano Novemba 18 ili kupata washindi wakatakaoenda Fainali.Kwa Afrika, Timu zinazogombea Nafasi hizo 3 ni ama Cameroun au Gabon toka KUNDI A, Tunisia au Nigeria toka KUNDI B, Misri au Algeria toka KUNDI C.
RATIBA:
Afrika
Novemba 14
Mozambique v Tunisia
Togo v Gabon
Morocco v Cameroun
Rwanda v Zambia
Kenya v Nigeria
Burkina Faso v Malawi
Ivory Coast v Guinea
Egypt v Algeria
Sudan v Benin
Novemba 15
Ghana v Mali
Marekani
Novemba 14
Costa Rica v Uruguay
Ulaya
Novemba 14
Urusi v Slovenia
Republic of Ireland v Ufaransa
Greece v Ukraine
Ureno v Bosnia-Herzegovina.


Tuesday, November 10, 2009

Da.!!FA yajaribu kumpa onyo Rooney kwa kauli: "MTU 12 MTU 12' aliyoitoa baada ya mechi ya Chelsea juzi!!!
wayne rooney
Mshambuliaji wa Manchester United Wayne Rooney amepewa onyo na FA, Chama cha Soka England, na ametakiwa achunge mwenendo wake wa baadae baada ya kunaswa akipiga kelele kwenye Kamera ya TV 'MTU 12!! MTU 12!!', akimaanisha Refa kawabeba Chelsea, mara tu baada ya mechi ya Ligi Kuu jana kumalizika huko Stamford Bridge kwa Chelsea kuifunga Man U 1-0 kwa goli la utata.Pia FA imesema Meneja wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, hana hatia baada ya kutamka maamuzi ya Refa Martin Atkinson yalikuwa ni upuuzi wa hali ya juu na pia kusema maamuzi kama hayo yanawafanya watu wakose imani kwa Marefa. Kwa sasa Ferguson yupo matatani na FA akikabiliwa na kesi inayosubiri uamuzi baada ya kushitakiwa mwezi Oktoba pale alipodai Refa Alan Wiley hayuko fiti kuchezesha mara tu baada ya mechi kati ya Man U na Sunderland kwisha dro 2-2.

Sunday, November 8, 2009

Boss Wa England Fabio Capello Ajalibu Kuwaonya Majeruhi!!!

Yule Boss wa England, Fabio Capello, amesema Kikosi chake hakina nafasi kwa Mchezaji ambae hayuko fiti na wasitegemea watachukuliwa kwenda Fainali Kombe la Dunia huko Afrika Kusini Juni mwakani ikiwa hawakuthibitisha uimara wao.Capello anategemewa kutangaza Kikosi chake kitakachocheza mechi ya kirafiki na Brazil Jumamosi tarehe 14 Novemba 2009 huko Doha, Qatar muda wowote leo.Capello amemzungumzia Rio Ferdinand na kusema ikiwa atakuwa fiti kabla hajateua Kikosi chake cha mwisho basi ataenda nae Afrka Kusini lakini ameonya kuwa Ledley King, Beki wa Tottenham, na Kipa David James wana mashaka makubwa kutokana na kuwa majeruhi.Kuhusu David James, Capello alisema: "James anacheza vizuri lakini tangu aumie akicheza mechi baadae hawezi kufanya mazoezi siku mbili.

Jinsi Nilivyomuumba Mke Ninayemtaka"

Dokta Reza Vossough alichukia maumbile ya mwanamke aliyetaka kumuoa lakini aliamua kumuoa ili amfanyie operesheni kibao za kubadilisha maumbile yake awe kama alivyopenda yeye mke wake awe.







Daktari wa operesheni za urembo za kurekebisha maumbile wa nchini Ujerumani Reza Vossough, amejitamba jinsi alivyomuoa mwanamke asiye na mvuto wowote na kumfanyia operesheni kila kona ya mwili wake kumgeuza mwanamke mwenye mvuto kwa jinsi alivyotaka yeye. Pichani Cany Vossough alivyo sasa baada ya operesheni kibao za kurekebisha maumbile yake. Gonga Life Style Pembeni kushoto kusoma habari kamili.






lil Wayne At The Miami Heat game with


got some pictures of Lil Wayne at the Miami Heat verses Denver Nuggets game with Common. You can see some photo this:

Saturday, October 31, 2009

NILIVYO ONA NILISHTUKA NIKA SEMA SIWEZI KUSITAJABU MIMI KUNA WADAUS






Mwanamke Ameza Uma na Vijiko 78Seti ya vijiko na uma vilivyotolewa toka kwenye tumbo lake

Uma ukitolewa toka kwenye tumbo lake wakati wa operesheni pembeni kulia ni baadhi ya vijiko na uma vilitolewa toka kwenye tumbo lake.

Madaktari nchini Ujerumani ilibidi wamfanyie operesheni ya dharura mwanamke mmoja aliyetambulika kwa jina la Margaret Daalman ambaye alikuwa akimeza vijiko na uma kila alipokuwa akila kwa muda mrefu kiasi cha kwamba jumla ya vijiko na uma 78 vilitolewa toka kwenye tumbo lake. Pichani Lundo la vijiko na uma vikiwa vimekusanyika kwenye tumbo lake. GONGA LIFE STYLE kwa habari zaidi.

Arsenal wawatoa nishai jirani zao Tottenham!!Arsenal 3 Tottenham 0

Katika dabi ya Timu za Kaskazini ya London, Arsenal wakiwa kwao Emirates Stadium waliwapiga Tottenham mabao 3-0 kwenye mechi ya Ligi Kuu iliyoanza mapema kuliko mechi nyingine za leo Jumamosi Oktoba 31.Mpaka mapumziko Arsenal walikuwa mbele kwa bao 2-0 kwa mabao yaliyofungwa ndani ya dakika moja katika dakika ya 43 Mfungaji akiwa Van Persie na la pili sekunde chache baadae kwa bao zuri sana la Nahodha Fabregas. Bao la 3 alifunga Van Persie.Vikosi:Arsenal: Almunia, Sagna, Gallas, Vermaelen, Clichy, Fabregas, Song Billong, Diaby, Bendtner, van Persie, Arshavin. AKIBA: Mannone, Senderos, Nasri, Eduardo, Ramsey, Eboue, Gibbs. Tottenham: Gomes, Corluka, King, Bassong, Assou-Ekotto, Bentley, Huddlestone, Palacios, Jenas, Keane, Crouch. AKIBA: Button, Hutton, Bale, Pavlyuchenko, Dawson, Kranjcar, Woodgate. Refa: Mark Clattenburg .

Monday, October 26, 2009

Milan certain of Beckham deal


David Bekham.
AC Milan vice-president Adriano Galliani is "100% certain" David Beckham will return to the San Siro outfit in the winter transfer market.
The England midfielder has been strongly linked with a second loan spell at the Rossoneri to improve his chances of making Fabio Capello's FIFA World Cup™ squad.
Galliani told the Italian media: "Beckham's arrival is certain to happen, 100%. The agreement is done and all that is missing are the signatures."
The 34-year-old Beckham returned to the Los Angeles Galaxy in the summer after a successful six-month loan spell with Milan, where he helped the Rossoneri finish fourth in Serie A with two story by
www.fifa.com

Lil Wayne – Run This Town [No Ceilings]


Holy shit, this is some sick Lil Wayne right here! Weezy goes in over Jay-Z’s “Run This Town” beat and absolutely murders it! This track is also from the No Ceilings mixtape which is dropping in 6 .

Wednesday, October 21, 2009

Fergie asusa Mkutano na Waandishi baada ya swali kuhusu Refa Wiley!!

Meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson aligoma kuendelea na mkutano wa Waandishi wa Habari uliokuwa ukifanyika Uwanjani Luzhniki huko Moscow, Urusi baada ya kuulizwa swali kuhusu kesi yake na FA iliyotokana na kauli yake kuwa Refa Alan Wiley hayuko fiti.Ferguson amepewa na FA mpaka Novemba 3 kuwasilisha utetezi wake kuhusu mashitaka yanayohusiana na kesi hiyo.Baada ya kuulizwa swali kuhusu Refa Alan Wiley, Ferguson aliinuka na kutoka chumba cha mahojiano baada ya kutamka: “Swali la kipumbavu na halipati jibu! Nipo kwenye mkutano huu kuhusu mechi na CSKA Moscow!”
NI USIKU WA MAAJABU ULIKUWA JANA BARANI ULAYA!!!
MASKINI: Liverpool ni vipigo mfululizo!!!! Barca waaibishwa Nou Camp!!!
echi za jana za UEFA CHAMPIONS LEAGUE zimeleta matokeo yasiyotarajiwa na magoli bwelele huku ajabu kubwa ni pale Warusi Rubin Kazan walipowakung’uta Mabingwa Watetezi wa Ulaya FC Barcelona kwa bao 2-1 tena wakiwa nyumbani kwao Nou Camp.

Liverpool wameendelea kupata vipigo mfululizo ingawa jana sio puto ndio liliwafunga bali ni goli la dakika za majeruhi wakiwa kwenye ngome yao Anfield na pia kupata athari kubwa pale mhimili wao na Nahodha wao Steven Gerrard kucheza dakika 25 tu za mwanzo na kulazimika kutoka baada ya kuumia.
Matokeo ya mechi ya jana ambayo Liverpool alifungwa 2-1 na Lyon ya Ufaransa yamedhihirisha ile imani ya wengi kuwa Liverpool bila Gerrard na Torres ni nyanya tu. Jana Torres hakucheza kabisa.
Sasa, baada ya vipigo mfululizo, Jumapili kwenye Ligi Kuuu, Liverpool wanawakaribisha Mahasimu wao wakubwa Manchester United na hilo linawatia homa Mashabiki wa Liverpool.
Arsenal wakiwa ugenini huko Uholanzi na huku wakiongoza bao 1-0 walilazimishwa sare ya 1-1 na AZ Alkmaar.
Rangers ya Scotland iliadhiriwa vibaya ikiwa nyumbani baada ya kuchapwa bao 4-1 na Unirea Urziceni.
Sevilla, baada ya mechi 3 tu, wameweka rekodi huko Ulaya baada ya kufuzu kusonga mbele Raundi nyingine baada ya mechi 3 tu.
Matokeo kamili mechi za jana Jumanne, Oktoba 20:
KUNDI E
Liverpool 1 Lyon 2
Debrecen 3 Fiorentina 4
KUNDI F
Inter Milan 2 Dynamo Kiev 2
Barcelona 1 Rubin Kazan 2
KUNDI G
Stuttgart 1 Sevilla 3
Rangers 1 Unirea Urziceni 4
KUNDI H
AZ Alkmaar 1 Arsenal 1
Olympiakos 2 Standard Liege 1

Monday, October 12, 2009

Big Brother Revolution: Images from Day 35 - SUNDAY OCTOBER 11


Day 35 on M-Net’s Big Brother was all action on the Sunday show with the evictions of Hannington and Yacob PLUS the exit of SuperSport celebrity guest Thomas Mlambo AND a performance by Kenya’s award-winning star Amani. Tune in to Big Brother Revolution on DStv channel 198 or 199 for more entertainment 24/7 live. For more information log on to Pictured here are Elizabeth and Kevin.