Thursday, September 3, 2009

LILE DIRISHA LA UHAMISHO LAFUNGWA!!!
Dirisha la Uhamisho lilifungwa rasmi Jumanne, Septemba 1 saa 1 usiku, saa za bongo, na Klabu za Ligi Kuu England zilitumia jumla ya Pauni Milioni 450 kununua Wachezaji, wakati msimu uliokwisha kipindi kama hiki zilitumia Pauni Milioni 500, na Klabu iliyoongoza katika manunuzi hayo ni Manchester City iliyotumia Pauni Milioni 120 ikiwa ni asilimia 27 ya jumla ya manunuzi ya Wachezaji kwa kununua Wachezaji 9.Klabu za Aston Villa, Liverpool, Sunderland na Tottenham zilitumia Pauni Milioni 25 kila mmoja kununua Wachezaji.Dirisha litakuwa wazi tena Januari 1, 2010.

No comments:

Post a Comment