Tuesday, September 15, 2009

UEFA yafuta kifungo cha Eduardo, huru kucheza kesho UEFA CHAMPIONS LEAGUE!!!

Rufaa ya Arsenal waliyokata kwa UEFA kupinga kwa adhabu ya Mshambuliaji wao mwenye asili ya Brazil lakini ni raia wa Croatia, Eduardo, aliyopewa kwa kumhadaa Refa Manuel Gonzalez katika mechi ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE na Celtic hapo Agosti 26, imekubaliwa na UEFA na sasa adhabu ya kufungiwa mechi mbili imefutwa.Eduardu sasa ni ruksa kucheza mechi ya kesho ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE ugenini Ubelgiji wakati Arsenal watakapokwaana na Standard Liege Uwanja wa Maurice Dufrasne.
yuleNahodha wa Everton Phillip Neville nje muda mrefu!!
Nahodha wa Everton, Phillip Neville, ambae ni mdogo wake Nahodha wa Manchester United, Gary Neville, atakuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu baada ya kuumia goti walipogongana na Dickson Etuhu wa Fulham katika mechi ya LIGI KUU siku ya Jumapili Uwanjani Craven Cottage na Fulham kushinda 2-1.Meneja wa Everton David Moyes amethibitisha habari hizo na kusema Neville ataenda kwa Wataalam Jijini London kwa uchunguzi zaidi na hapo ndipo watajua kwa uhakika muda gani atakosekana.

No comments:

Post a Comment