Thursday, September 10, 2009

0, Paraguay waingia Fainali!!!


Paraguay leo alfajiri wameungana na Brazil kutoka Nchi za Marekani ya Kusini kuingia Fainali za Kombe la Dunia baada ya kuwapa kipigo cha bao 1-0 Argentina kwenye mechi iliyochezwa Paraguay.
Jumamosi, Argentina wakiwa nyumbani Rosario City, walipigwa bao 3-1 na Mahasimu wao wakubwa Brazil.
Bao la Paraguay lilifungwa na Haedo dakika ya 28.
Kwa kipigo hiki cha pili mfululizo ambacho mbali ya kuhatarisha sana nafasi ya Argentina kucheza Fainali huku zikiwa zimebaki mechi 2 tu kwenye Kundi lao, hata kibarua cha Kocha Diego Maradona sasa kina walakini mkubwa

No comments:

Post a Comment