Wednesday, September 9, 2009

David Gill wa Man U kachaguliwa katka chama cha Klabu Ulaya [ECA]!

Mkurugenzi Mkuu wa Manchester United, David Gill, amechaguliwa kwenye Bodi ya Chama cha Klabu Ulaya, ECA, [European Club Association] pamoja na Rais wa Real Madrid, Florentino Perez kwa kipindi cha miaka miwili.
ECA ina Bodi hiyo yenye Wawakilishi 15 na hupeleka Wajumbe wake kwenye Kamati za UEFA na kushirikiana na kutoa ushauri kuhusu masuala ya Soka huko Ulaya.
ECA inaundwa kutokana na Klabu 144 toka Nchi 53 za Ulaya na hupigania haki za Vilabu hivyo huko Ulaya.

No comments:

Post a Comment