Wednesday, September 2, 2009

Ranieri ateuliwa Maneja Roma huko Italia!!!

Ranieri
Meneja wa zamani wa Chelsea Claudio Ranieri, miaka 57, ameteuliwa kuwa Bosi mpya wa AS Roma ambayo iko Serie A huko Italia kuchukua nafasi ya Luciano Spalletti aliejiuzulu Jumanne iliyopita.Spalletti alichukua hatamu hapo AS Roma mwaka 2005 na kuiwezesha kushinda Kombe la Italia na kushika nafasi ya pili Serie A mwaka 2007 na 2008 lakini msimu uliopita walimaliza nafasi ya 6 na hivyo kukosa kucheza UEFA CHAMPIONS LEAGUE na badala yake wako EUROPA LIGI.Msimu huu katika mechi 2 za Ligi, Roma imefungwa zote na hilo likamfanya Spalletti ang’atuke.Ranieri aliiongoza Chelsea kati ya mwaka 2000 na 2004 na hivi karibuni alikuwa Juventus lakini akatimuliwa mwezi Mei baada ya Timu hiyo kucheza mechi 7 mfululizo bila ushindi.

No comments:

Post a Comment