Thursday, September 3, 2009

Sammy Lee apewa onyo na FA!!!!

Sammy Lee
Meneja msaidizi wa Liverpool, Sammy Lee, amepewa onyo na FA baada ya kukiri kosa la utovu wa nidhamu alipomkashifu Mwamuzi wa Akiba, Stuart Attwell, katika mechi ya Ligi Kuu kati ya Tottenham na Liverpool ambayo Liverpool walifungwa 2-1 na Sammy Lee kukasirishwa na Refa Phil Dowd kutowapa penalti.Sammy Lee, katika mechi hiyo, alitolewa uwanjani na Refa Phil Dowd baada ya kufarakana na Mwamuzi huyo Stuart Attwell.Kamisheni iliyosikiliza kesi hiyo ya Sammy Lee haikumpa adhabu kali kwa kuwa rekodi yake ni nzuri.Vilevile, Meneja wa Liverpool, Rafa Benitez, nae pia anayo kesi kwenye Kamisheni hiyo akituhumiwa kumkashifu Refa mara baada ya mechi hiyo hiyo na Tottenham.


No comments:

Post a Comment