Sunday, September 13, 2009

van persie adai emmanuel alimtimba makusudi ili amumize...!!!


Van Persie adai Adebayor alimtimba makusudi amuumize!!!=Adebayor huenda akasulubiwa na F.A kwa ushangiliaji!!!!

Emmanuel Adebayor, aliefunga bao moja dhidi ya Timu yake ya zamani Arsenal katika mechi ya jana ambayo Manchester City iliipiga Arsenal 4-2, huenda akawa matatani na FA hasa baada ya kufunga goli hilo la 3 na kisha kukimbia nusu ya Uwanja na kwenda mbele ya Mashabiki wa Arsenal kushangilia kitendo ambacho Refa alimpa Kadi ya Njano.Mashabiki hao wa Arsenal walichukizwa sana na kitendo hicho na ilibidi Polisi na Walinzi wawatulize.Ndani ya uwanja, Mchezaji wa Arsenal, Robben van Persie amedai Adebayor alimkanyaga usoni makusudi ingawa Adebayor mwenyewe amekiri hilo lakini amesema ni bahati mbaya na alimwomba radhi van Persie.Kitendo hicho hakikuonekana na Refa lakini van Persie amepinga kuwa Adebayor alimwomba radhi na aliendelea kung’ang’ania alitimbwa kusudi.

No comments:

Post a Comment