Wednesday, August 19, 2009

Arsenal ushindi tu.



UEFA CHAMPIONS LEAGUE: Arsenal yaipiga Celtic 2-0 nyumbani kwao!!
Arsenal jana walianza vyema harakati zao za kutaka kuingia hatua ya Makundi ya UEFA Champions League baada ya kuibugiza Celtic ya Scotland hukohuko kwao Uwanjani Parkhead kwa mabao 2-0.
Timu hizi zitarudiana wiki ijayo Jumanne Emirates Stadium nyumbani kwa Arsenal.
Matokeo mechi nyingine za UEFA CHAMPIONS LEAGUE zilizochezwa jana ni: [kwenye mabano ni Nchi Timu zinazotoka]
FC Sheriff Tiraspol [Moldova] 0 Olympiacos [Greece] 2
Celtic [Scotland] 0 Arsenal [England] 2
Poli Aek Timisoara [Romania] 0 VfB Stuttgart [Germany] 2
FC Kobehavn [Denmark] 1 APOEL Nicosia FC [Cyprus] 0
Sporting Lisbon [Portugal] 2 Fiorentina [Italy] 2

LIGI KUU ENGLAND: Chelsea wachanja mbuga!
Jana Chelsea wameendeleza wimbi lao la ushindi baada ya kushinda ugenini walipoipiga Sunderland mabao 3-1 mabao yote matatu yakifungwa kipindi cha pili baada ya Sunderland kuongoza kwa bao lililofungwa na Darren Bent hadi mapumziko.
Mabao ya Chelsea yalifungwa na Ballack, Lampard [penalti] na Deco.
Katika mechi nyingine za LIGI KUU, Wigan wakiwa nyumbani walipachikwa kimoja na Wolverhampton timu iliyopanda Daraja msimu huu.
Mechi za leo LIGI KUU ni: [saa za bongo]
-SAA 3 DAK 45 usiku
Birmingham v Portsmouth
Burnley v Manchester United
Hull City v Tottenham
-SAA 5 usiku
Liverpool v Stoke City

No comments:

Post a Comment