Friday, August 21, 2009

EUROPA LEAGUE

EUROPA LEAGUE: Everton na Fulham zapeta mechi ya kwanza nyumbani, Villa yapigwa kimoja ugenini!!!
Kwenye mechi za kwanza za mchujo wa kuwania kuingia kwenye Makundi ya EUROPA LEAGUE Klabu za England Aston Villa, Everton na Fulham, zilizomaliza LIGI KUU England zikiwa nafasi za 5, 6 na 7 na hivyo kupata nafasi kucheza Ulaya, leo zilitupa karata zao na ni Aston Villa pekee waliocheza ugenini walifungwa bao 1-0 na Rapid Vienna ya Austria huku Everton na Fulham zikipata ushindi mnono kwao.
Everton waliibamiza Sigma Olomouc ya Urusi kwa mabao 4-0 mawili mguuni kwa Luis Saha na mengine mawili toka kwa Chipukizi Jack Rodwell.
Fulham waliinyuka Amkar Perm ya Urusi 3-1 kwa mabao ya Jonhson, Dempsey na Zamora.
Marudiano ya mechi hizi ni wiki ijayo.
Matokeo mengine ni:
Ajax 2 Bratislava 0
CSKA Sofia 0 Dinamo Moscow 0
FC Twente 3 FK Qabarag 1
Guingamp 1 Hamburg 5
MFK Kosice 3 Roma 3.

No comments:

Post a Comment