Monday, August 31, 2009

LIGI KUU ENGLAND kusitishwa wiki 2 kupisha Mitoano KOMBE LA DUNIA!!!

Baada ya kuchezwa mechi za jana Jumapili, LIGI KUU itasimama kwa wiki mbili na kurudi tena tarehe 12 Septemba 2009 ili kupisha mechi za Timu za Taifa za kuwania nafasi za kuingia Fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini mwakani.Mechi hizo za Mataifa zitachezwa tarehe 5 Septemba na tarehe 9 Septemba.RATIBA YA LIGI KUU ni kama ifuatavywo:JUMAMOSI, 12 Septemba 2009 [SAA ZA BONGO][saa 11 jioni]Blackburn v WolverhamptonLiverpool v BurnleyMan City v ArsenalPortsmouth v BoltonStoke v ChelseaSunderland v HullWigan v West ham[saa 1 na nusu usiku]Tottenham v Man UJUMAPILI, 13 Septemba 2009[saa 8 mchana]Birmingham v Aston Villa[saa 12 na robo]Fulham v Everton.KikoCapello ateua si cha England!! Kocha wa England Fabio Capello ametangaza Kikosi chake kitakachopambana na Slovenia kwa mechi ya kirafiki hapo Jumamosi na mechi ya mtoano wa Kombe la Dunia dhidi ya Croatia Jumatano Septemba 5.Peter Crouch, Aaron Lennon na Wes Brown wameitwa tena Kikosini baada ya kukosekana katika mechi za hivi karibuni za Timu hiyo.Lakini Mshambuliaji wa Manchester United Michael Owen hakuitwa pamoja na Maveterani wa Timu hiyo Kipa David James na Mlinzi Rio Ferdinand ambao ni majeruhi.England watacheza na Slovenia Wembley saa moja na nusu usiku, saa za bongo, hapo Jumamosi, na Jumatano, Septemba 5 mechi na Croatia itakuwa saa 4 usiku saa za bongo.Endapo England wataifunga Croatia hiyo Jumatano watajihakikishia kucheza Fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini mwaka 2010.KIKOSI KAMILI:Makipa: Foster (Manchester United), Green (West Ham), Robinson (Blackburn)Walinzi: Johnson (Liverpool), Brown (Manchester United), Upson (West Ham), Terry (Chelsea), Lescott (Manchester City), A Cole (Chelsea), Bridge (Manchester City)Viungo: Wright-Phillips (Manchester City), Lennon (Tottenham), Beckham (Los Angeles Galaxy), Barry (Manchester City), Lampard (Chelsea), Carrick (Manchester United), Gerrard (Liverpool), A Young (Aston Villa), Milner (Aston Villa)Washambuliaji: Rooney (Manchester United), Heskey (Aston Villa), Defoe (Tottenham), C Cole (West Ham), Crouch (Tottenham

No comments:

Post a Comment