Friday, August 21, 2009

Lampard: "Ni Messi tu anaweza kumbadili Ronaldo!"

Kiungo wa Chelsea Franck Lampard amesema Manchester United hawawezi kupata mbadala wa Cristiano Ronalndo labda wamchukue Messi.
Hata hivyo Lampard amesema anaamini pengo la Ronaldo litazibwa kwa Meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson kuifanya Timu hiyo icheze "kitimu" badala ya kutegemea mtu mmoja na hivyo amekiri Man U itakuwa tishio.
Rio nje mwezi!!
Taarifa zinasema Beki kigogo wa Manchester United, Rio Ferdinand, atakuwa nje ya uwanja mwezi mzima baada ya kuumia musuli pajani mazoezini.
Hivyo Ferdinand ataikosa mechi ya Jumamosi hii dhidi ya Wigan na Jumamosi ijayo dhidi ya Arsenal.

No comments:

Post a Comment